Monday, January 30, 2017

MWENYEKITI CCM MBEYA APIGWA RISASI.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Wilaya ya Mbeya Ephreim Mwaitenda amejeruhiwa kwa risasi baada ya watu wasiojulikana kuvunja dirisha na kuchana nyavu za dirisha katika eneo la shamba lake wilayani Kyela kisha kupenyeza mtutu na kumpata Mwaitenda mgongoni na kusababisha baadhi ya risasi kukwama katika mwili wake eneo la mgongo.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Emmanuel Lukula amesema Mwaitenda alipigwa risasi majira ya saa nane usiku januari 30 mwaka huu kwa risasi za goroli na bunduki iliyotengenezwa kienyeji na majeruhi amekimbizwa hospitali ya Wilaya ya Kyela kabla ya kuhamishiwa rufaa Mbeya . Lukula amesema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kuwabaini wahusika na katika eneo la tukio baadhi ya vitu vimeokotwa vitavyosaidia uchunguzi. Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Zongo Lobe Zongo baada ya kupata taarifa amesema walifanikiwa kumsafirisha majeruhi hadi hospitali ya rufaa Mbeya. Aidha amewapongeza Polisi kwa kufika haraka eneo la tukio na Madaktari ambao wanafanya juhudi za kuondoa risasi zilizokwama mgongoni. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya Dr Godlove Mbwanji amesema wamempokea majeruhi huyo ambapo walimfanyia X-ray na wakati wowote walimfanyia upasuaji kuondoa risasi zilizokwama mgongoni.



MZIGO WA LIGI KUU ENGLAND KATIKATI YA WIKI HII HUU HAPA


JUMANNE Januari,31, 2017


Show last 5 matches and coverageFixtureKick-offStatus
22:45
22:45
22:45
22:45
22:45
22:45
23:00

JUMATANO  Februari,1, 2017


Show last 5 matches and coverageFixtureKick-offStatus
22:45
23:00
23:00

YANGA YAPAA KILELENI,MSIMAMO HUU HAPA.


Saturday, January 21, 2017

MOURINHO:HAKUNA BEKI BORA KAMA VALENCIA


Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema haoni beki bora wa kulia zaidi ya Antonio Valencia
Jose Mourinho amesema beki wa Manchester United Antonio Valencia ni beki bora zaidi wa kulia katika mpira wa miguu.
United waliboresha mkataba wa mchezaji huyo kwa kumwongezea mwaka mmoja ili kumfunga klabuni hapo hadi 2018.
Awali alisajiliwa kama winga 2009, Valencia amejiimarisha na kuwa mchezaji muhimu zaidi katika safu ya ulinzi ya Mourinho, akifanikiwa kuanza mechi 23 katika michuano yote.
Na Mourinho amefurahishwa na kiwango cha mchezaji huyo, ambaye anaamini anayo kila sababu ya kusifiwa kwa mchango wake na alistahili dili jipya.
 “Sidhani amepata dili jipya kama thawabu, silioni jambo hili kwa mtazamo huo,” Mourinho alikiambia MUTV.
“Nadhani ni beki bora zaidi wa kulia kwa sasa. Hakuna beki bora zaidi yake katika soka. Ni haki yetu kumbakisha mchezaji mahiri. Sioni kama ni thawabu, amestahili.
“Ni kipaumbele chetu kuwa na wachezaji bora na mtu mwema kama yeye.
“Antonio anacheza vizuri mno, nadhani. Msimu huu anacheza katika kiwango kikubwa ajabu.”
 “Hakuwa akicheza kama beki wa kulia, mimi nimemtaka kucheza nafasi ya beki wa kulia,”  meneja huyo alieleza jinsi alivyoshindwa kumchukua mchezaji huyo alipokuwa Real Madrid Hispania.
“Lakini Manchester United walikuwa imara na wenye akili. Walizuia kila uwezekano wa kumpoteza.”
Heshima kubwa za Valencia katika Old Trafford ni pamoja na mataji mawili ya Ligi Kuu, mnamo 2011 na 2013, kadhalika Kombe la FA na Medali za Kombe la EFL.

THOMAS ULIMWENGU APATA ULAJI ULAYA

Ulimwengu ataingia kikosi cha kwanza moja kwa moja na kazi yake kubwa itakuwa ni kuhakikisha timu hiyo inabeba ubingwa wa ligi kuu
Hatimaye mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Thomas Ulimwengu, amejiunga na klabu ya Athletic Football Club Eskilstuna ya Sweden kwa mkataba wa miaka miwili.
Meneja wa Ulimwengu Jamali Kisongo, ameiambia Goal, timu hiyo imemsajili Ulimwengu kwa mkataba wa miaka miwili na anatarajiwa kuanza kuitumikia timu hiyo hivi karibuni.

“Ni kweli tumekamilisha mkataba wa miaka miwili ya klabu ya Athletic Football Club Eskilstuna ,mimi na Ulimwengu tunatarajia kwenda Sweden, kwa ajili ya kukamilisha baadhi ya mambo ikiwemo vibali vya kufanyia kazi na nyumba ya kuishi,” amesema Kisongo.

Mshambuliaji huyo aliyetamba na TP Mazembe ya DR Congo, amesema timu hiyo kwa muda mrefu ilikuwa ikimfatilia, Ulimwengu na hata baada ya kumaliza mkataba wake ili ilitaka kumsajili lakini ilishindakana kwakua kipindi cha usajili kilikuwa bado hakijafika.

Amesema Athletic Football Club Eskilstuna ni moja kati ya timu kubwa nchini Sweden, hivyo kama ulimwengu atapambana anaweza kufika mbali na kuweza kuonekana na timu kubwa na kuweza kusajiliwa.

“Tunashukuru kwa mpango huo kukamilika nafikiri kilichobaki ni kwa mchezaji mwenye aweze kuonyesha juhudi kwa kupambana ili aweze kujitengenezea mazingira ya kusajiliwa na timu kubwa za ndani na nje ya Sweden,”amesema Kisongo.

Meneja huyo amesema anaimani kubwa na mteja wake, kuwa hatomuangusha kama ilivyo kwa Mbwana Samatta, ambaye anatamba na KRC Genk ya Ubelgiji.

Amesema Ulimwengu kabla ya kuamua kutua Sweden, alikuwa na ofa nyingi mkononi zinazo mhitaji mchezaji huyo lakini ofa ya Sweden ndiyo ilikuwa yakuvutia zaidi na ndiyo maana wakaamua kuikubali.

Kwamujibu wa Kisongo, Ulimwengu ataingia kikosi cha kwanza moja kwa moja na kazi yake kubwa itakuwa ni kuhakikisha timu hiyo inabeba ubingwa wa ligi kuu ya taifa hilo ambayo inashirikisha timu 16 na inatarajiwa kuanza kutimua vubmi Aprili mwaka huu.

CONTE:AKE ATAIPA UBINGWA CHELSEA


Antonio Conte anaamini Nathan Ake anaweza kuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Chelsea duru la pili Ligi Kuu Uingereza msimu huu
Nathan Ake anayo nafasi ya kuisaidia Chelsea katika mbio za ubingwa Ligi Kuu kwa mujibu wa meneja wa klabu hiyo Antonio Conte.
Beki Ake ameitwa kutoka Bournemouth alipokuwa akitumika kwa mkopo mwezi huu baada ya kuonyesha uwezo mkubwa katika kikosi cha Eddie Howe.
Na Conte amesisitiza kuwa Mdachi huyo amerejeshwa klabuni mwake dirisha la uhamisho Januari si kwa ajili ya matakwa ya kifedha kwa kutaka kumuuza, la!
Badala yake, Muitaliano huyo anaamini Ake kama mchezaji mahiri atakuwa mchezaji muhimu kuisaidia Chelsea kuendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi na hata kutwaa taji.
“Nathan Ake amerudi kwenye kikosi chetu kwa sababu nimethaminisha hali yake na hali yetu na anaonekana kuwa na ari,” Conte aliwaambia waandishi kwenye mkutano.
“Ake ni mchezaji anayeweza kucheza kwenye nafasi tofauti-tofauti. Nadhani ameimarika sana na sasa yupo tayari kucheza kwenye kikosi cha Chelsea na atatusaidia.
“Hii ni wiki ya pili amekuwa nasi na ameanza kuelewa falsafa yetu ya mpira. Napendezwa naye.”
Jumapili Chelsea watawakabili Hull City ambao wapo kwenye kipindi kigumu Ligi Kuu.

Jammeh "kuachia madaraka na kuondoka"


Kiongozi wa Gambia Yahya Jammeh atawachia madaraka na kuondoka nchini Gambia, kwa mujibu wa maafisa wanaongoza mapatano.

Wapatanishi wa Afrika Magharibi watliumia masaa kadha wakikutana na bwana Jammeh siku ya Ijumaa kuzungumzia hatma yake.

Msafara wa magari uliowabeba marais wa Guinea na Mauritania, umeondoka makao ya Jammeh lakini hayaaminiwi kuondoka nchi humo.

Bwana Jammeh alishindwa kwenye uchaguzi wa mwezi Disemba na mrithi wake Adama Barrow ameapishwa.

Jammeh alikuwa amepewa makataa ya kuondoka madarakani kufikia saa sita mchana la sivyo aondolewe kwa nguvu na wanajeshi wanaoungwa mkono na UMoja wa Mataifa.

MZAZI ASIMULIA MAITI YA MTOTO ALIVYOACHWA CHUMBANI

Mbeya.  Mzazi Jailo Kyando (36), ambaye maiti ya mtoto wake iliachwa chumbani na waombolezaji ambao walizika jeneza tupu, amesema huenda wabebaji walitegeana hivyo kutong’amua kuwa halikuwa na mwili wa marehemu.

Mtoto huyo, Haruna Kyando (9), aliyekuwa akisumbuliwa na kifafa kwa muda mrefu, alikutwa chumbani asubuhi ya Jumatatu akiwa amefariki dunia nyumbani kwao Isanga mjini hapa, baadaye waombolezaji waliamua kumzika bila  kutoa heshima za mwisho.

Lakini, baada ya jeneza kupelekwa nyumbani kwa ajili ya kuweka maiti ya mtoto huyo, waombolezaji hawakushughulika na mwili badala yake, walibeba jeneza na kuungana na wengine kwenda kulizika, lakini waliporudi nyumbani, walikuta maiti juu ya godoro hilo kama ilivyokuwa imewekwa kabla ya kwenda makaburini.

Akisimulia tukio hilo, mzazi huyo alisema kifo cha ghafla cha mwanaye kiliwachanganya yeye na mkewe, Anna Elieza (32)  hadi kufikia kushindwa kufanya jambo lolote.

Tuesday, January 17, 2017

YANGA YAPATA USHINDI SONGEA BAADA YA MIAKA 30


YANGA SC imevunja mwiko wa kutoshinda Uwanja wa Maji Maji mjini Songea kwa miaka 30 baada ya jioni ya leo kuwafunga Maji Maji 1-0 kwenye Uwanja huo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Ushindi huo unawafanya mabingwa hao watetezi, Yanga wafikishe pointi 43 baada ya kucheza mechi 19, ingawa inaendelea kukaa nafasi ya pili nyuma ya vinara Simba SC wenye pointi 44 za mechi 18.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Hussein Athumani aliyesaidiwa na Mirambo Tshikungu na Vincent Mlabu, hadi mapumziko Yanga walikuwa tayari mbele kwa bao hilo moja.
Bao hilo lilifungwa na kiungo Deus Kaseke dakika ya 14 aliyefumua shuti zuri baada ya kukutana na mpira uliopanguliwa na kipa Agathon Anthony kufuatia krosi maridadi ya Nahodha, Haruna Niyonzima.
Baada ya bao hilo, Maji Maji nao wakafunguka na kuanza kushambulia moja kwa moja langoni mwa Yanga, lakini safu ya ulinzi ya wana Jangwani iliyoongozwa na nguli Kevin Yondan ilisimama imara kudhibiti hatari zote.
Yanga ingeweza kumaliza kipindi cha kwanza inaongoza kwa mabao zaidi kama ingetumia vizuri nafasi zaidi, ikiwemo ile ya dakika ya pili tu baada ya kiungo Juma Mahadhi kujigonga gonga na mpira miguuni baada ya pasi nzuri ya mshambuliaji Amissi Tambwe kwenye boksi hadi beki Keneddy Kipepe akaokoa na kuwa kona iliyookolewa pia. 
Mapema dakika ya 25, kocha wa Maji Maji na mchezaji wa zamani wa Yanga, Kali Ongala alimtoa beki Bahati Yussuf na kumuingiza Emmanuel Semwanza aliyesajiliwa dirisha dogo Desemba kwa mkopo kutoka Maji Maji.
Na mwanzoni tu mwa kipindi cha pili, Ongala mtoto wa gwiji wa zamani wa muziki nchini, Dk. Remmy Ongala (sasa marehemu) akamuingiza Peter Mapunda kwenda kuchukua nafasi ya Lucas Kikoti.
Mabadiliko hayo, hayakuweza kuwasaidia Maji Maji, kwani pamoja na kupeleka mashambulizi mengi kwenye eneo la Yanga, hawakuchomoa bao. 
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa michezo miwili, Simba wakiwa wageni wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Azam FC wakiwa wenyeji wa Mbeya City Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
 

Monday, January 16, 2017

Breaking Newzz: Lowassa Akamatwa na Jeshi la Polisi Geita

Waziri Mkuu mstaafu na aliyekuwa mgombea urais kwa CHADEMA Mh. Edward Lowassa na mbunge wa Geita (M) Viti maalum Upendo Peneza wamekamatwa  na jeshi la Polisi Geita mjini.

Taarifa zinaarifu kuwa  Lowassa amefika Geita leo akitokea Kagera  ambapo alipofika stendi ya zamani Geita wananchi walimsimamisha. Aliposhuka kwenye gari kuwasalimu wanageita, polisi wakamkamata na kumpeleka kituo cha Polisi Geita.

Lowassa alikuwa anaenda kwenye kampeni za uchaguzi Kata ya Nkome

Hivi ndivyo vipigo vitakatifu alivyowai kupata Pep Gurdiola


Image result for pep guardiola
Pep Gurdiola na yeye ameingia kwenye mfumo wa 4G kama Yanga.Toka Pep aje Uingereza katika ligi kuu ya EPL Everton ndio wamempa kipigo kikubwa zaidi.Ameshafungwa goli 4 na Leicester City huku akipigwa 3 na Chelsea.Hii sio mara ya 1 kwa Pep kula kipigo cha mbwa mwizi,huko alikotoka ameshapigwa pigwa sana.Hizi ni mechi ambazo Pep alifungwa goli nyingi zaidi.

19/10/2016 Barcelona 4 – Man City 0.

Hii ilikuwa mechi ya UEFA katika hatua ya makundi.Pep alikuwa na miezi miwili toka aichukue Man City.Katika hatua za makundi City alikuwa kundi moja na Barcelona.Man City walisafiri kwenda Nou Camp kuwakabili Barcelona,katika mechi hiyo zidi ya timu yake ya zamani Gurdiola alikutana na dhahma hiyo huku Lioneil Messi akipiga hat trick na Neymar akifunga goli moja.

29/4/2014 Bayern Munich 0 – Real Madrid 4.

Hii ilikuwa nusu fainali ya UEFA,huku Bayern wakiwa na goli 1 walilolipata Santiago Bernabeu walihitaji suluhu tu kwenda fainali.Lakini Real Madrid wakiwa na nyota wao Cristiano Ronaldo walimshushia kipigo hicho Pep Gurdiola na kuitupa Bayern nje ya UEFA.Ni Sergio Ramos na Cristiano Ronaldo walipiga goli mbili kila mmoja na kumtupa nje ya mashindano hayo Pep Gurdiola.

30/1/2015 Wolfburg 4 – Bayern Munich 1.

Kelvin De Bruyne ambae sasa yuko na Gurdiola alifunga mara mbili na Bast Dost alifunga pia mara mbili.Hiki ni kati ya vipigo vikubwa alivyopata akiwa Bundesliga japo pamoja na kipigo ila aliibuka na kombe hilo.

12/4/2014 Bayern Munich 0 – Borrusia Dortmund 3.

Kipigo kingine kwa Gurdiola kilitoka kwa wapinzani wao wakubwa Ujerumani.Borrusia Dortmund waliichapa Bayern Munich ya Gurdiola goli 3 huku mchezaji wa sasa wa Manchester United Henrikh Miktaryan akifunga moja kati ya magoli hayo.Magoli mengine ya Dortmund yaliwekwa kimiani na Marco Reus na Jonas Hoffman.

15/1/2017 Everton 4 – Man City 0

Gurdiola toka ajiunge na Man City hii ni mara ya nne anafungwa goli nne katika mechi moja.Alifungwa na Leicester goli nne kwa mbili,alifungwa na Barcelona goli nne kwa bila na sasa anakufa mbele ya Everton tena goli nne kwa sifuri.Makinda mawili Adeemola Lookman aliyenunuliwa wiki iliyopita akitokea Charton na Tom Davies aliyepandishwa kutoka academy ya vijana walipeleka kilio City wakifunga goli moja moja.Kevin Miralass na Lukaku walitangulia kucheka na nyavu.

MSIMAMO LIGI KUU BARA



NA KENNEDY SIMUMBA


#TeamMPWDLFADPLast 5 matches
1181422306+2444WWWLL
2181242399+3040WDWWW
3Previous rank: 5199462018+231WLWDW
4Previous rank: 3188642315+830WDDWL
5Previous rank: 4188642319+430WWDWW
6Previous rank: 8196761816+225WLLLL
7Previous rank: 6186661616+024WDDLW
8Previous rank: 7195951820-224DLWDL
9185761013-322LLWWL
10196491624-822LWWWL
11194961116-521DDDDW
12195591724-720DLLWW
131954101326-1319LLLLW
141852111326-1317LDLWW
151844101120-916WDLDL
1619298717-1015DDLLD