Monday, November 28, 2016

DSS NEWS: HARUSI ILIYOFUNJA REKODI KATIKA WILAYA YA ILEJE

                                                                   MR & MRS
Harusi hiyo ilionekana kuwa na  watu wengi kuliko harusi zote zilizofanyika wilayani hapo
Ndugu Gwamaka Mbughi akiongea na DSS TV, Atoa shukran za pekee kwa wakazi wa Ileje
                                                 MZAZI WA ELIZABETH KILAWE


MZAZI WA GWAMAKA MBUGHI

 GWAMAKA MBUGHI NA ELIZABETH KILAWE

Friday, November 18, 2016

BAADA YA MAPUMZIKO YA MECHI ZA KIMATAIFA LIGI KUU ENGLAND KULINDIMA WIKIENDI HII,MZIGO WOTE NDANI YA SUPER SPORT


Related image
MARCUS RASHFORD

MUDA WOTE  NI AFRIKA MASHARIKI

JUMAMOSI,NOVEMBA,19,2016
Show last 5 matches and coverageFixtureKick-offStatus
15:30
Manchester United VsArsenal
18:00
Crystal Palace VsManchester City
18:00
Everton VsSwansea City
18:00
SouthamptonVs Liverpool
18:00
Stoke City VsBournemouth
18:00
SunderlandVs Hull City
18:00
Watford VsLeicester City
12:30
Tottenham Hotspur VsWest Ham United



JUMAPILI,NOVEMBA 20,2016

19:00
MiddlesbroughVs Chelsea

JUMATATU, Novemba,21, 2016


Show last 5 matches and coverageFixtureKick-offStatus
23:00
Arnautovic and Shaqiri

LIGI YA MKOA DARAJA LA TATU SONGWE KUUNGURUMA LEO

NA KENNEDY SIMUMBA,DSS TV,
Ligi daraja la kwanza inaendelea leo ambapo mchezo wa kukata na shoka utapigwa leo kati ya Ifad FC ya Songwe na Morning Star FC ya Tunduma.
Mechi hiyo itapigwa uwanja wa Ifuko Songwe jioni ya leo.Wadau wa mpira wa miguu y mkoa wa Songwe mnaombwa kuhudhuria mechi hiyo.

DSS TV: Dr. OBEDI SICHEMBE 13/11/2016

Thursday, November 17, 2016

SHUKURANI ZA DHATI KWA MAN CHENCHECHELE

Msanii wa mziki wa  Hip Hop wamewashukuru mashabiki wote waliomsapoti wakati wa show ya uzinduzi wa Albam yake iliyofanyika tarehe 13/11/2016 kwenye ukumbi wa Uwanji hill Mpemba.
Akizungumza na DSS TV Man Chenchechele amesema binafsi hana maneno mengi zaidi ya kuwashukuru wote waliojitoa kwa hali na mali kufanikisha uzinduzi huo.














Friday, November 11, 2016

RAIS MAGUFULI AONGOZA KUMUAGA SAMUEL SITTA NA ATUMA RAMBIRAMBI KIFO CHA MBUNGE HAFIDH ALI TAHIR

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akitoa heshima zake za mwisho kwa aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akimfariji Mama Margareth Sitta, Mjane wa aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 11 Novemba, 2016 amewaongoza viongozi na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samuel John Sitta aliyefariki dunia tarehe 07 Novemba, 2016 katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani.

Mwili wa Marehemu Samuel John Sitta umeagwa katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam ambapo Viongozi wengine waliojumuika kuuaga mwili huo ni pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Mawaziri wakuu wastaafu Jaji Joseph Sinde Warioba na Frederick Tluway Sumaye, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Jaji Kiongozi Mhe. Ferdinand Katipwa Wambali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

Baada ya kuagwa katika viwanja vya Karimjee, mwili wa Marehemu Samuel John Sitta umesafirishwa kwenda Dodoma ambako Wabunge, Viongozi wa Mkoa na wananchi watapata fursa ya kuuaga katika Viwanja vya Bunge na baadaye jioni utasafirishwa kwenda Tabora ambako maziko yatafanyika kesho Jumamosi huko Urambo.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Dimani Zanzibar Mhe. Hafidh Ali Tahir kilichotokea majira ya saa 9 usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.Mhe. Hafidh Ali Tahir amefariki dunia muda mfupi alipofikishwa hospitali baada ya kuugua ghafla.

"Nimeshtushwa sana na kifo cha Mhe. Hafidh Ali Tahir na ninakuomba Mhe. Spika Job Ndugai unifikishie salamu za pole kwa Familia ya Marehemu, Wabunge, Wananchi wa Jimbo la Dimani, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huu.

"Tutamkumbuka Mhe. Hafidh Ali Tahir kwa mchango wake mkubwa alioutoa katika utumishi wa umma, katika michezo na akiwa mwakilishi wa wananchi, kwa hakika tumepoteza mtu muhimu sana" amesema Rais Magufuli na kumuombea Marehemu apumzishwe mahali pema peponi. Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
11 Novemba, 2016
 Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe Benjamin William Mkapa na mkewe Mama Anna Mkapa wakitoa heshima  za mwisho kwa aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016
  Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akimpa pole binti wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akimpa pole Mhe. John Sitta, mtoto wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016

 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016.
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Nobemba 11, 2016
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . John Pombe Magufuli akiwapa pole wanafamilia  wa  aliyekuwa Spika Mstaafu Marehemu Samwel John Sitta alipoongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 11, 2016

MAJALIWA AONGOZA WABUNGE KUAGA MWILI WA MBUNGE WA DIMANI- HAFID HALLY TAHIR

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Mbunge wa Dimai Hafidh Ally Tahir, bungeni mjini Dodoma Novemba 11, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Spika wa Bunge, Job Ndugai akitoa heshima za mwisho kwa mbunge wa Dimani, marehemu Hafidh Ally Tahir kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Novemba 11, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kwa mbunge wa Dimani, Hafidh Ally Tahir kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Novemba 11, 2016. Mbunge huyo alifariki dunia mjijini Dodoma usiku wa kuamkia leo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai (kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Walemavu, Jenista Mhagama (wapili kulia) na Katibu wa Bunge, Dkt.Thomas Kashililah wakisubiri kupokea mwili wa Mbunge wa Dimani, marehemu Hafidh Ally Tahir kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma ambako ulisafirishwa kwenda Zanzibar kwa Mazishi Novemba 11, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai na Kiongozi wa Upinzania bungeni, Freeman Mbowe (kulia) wakishuhudia wakati mwili wa mbunge wa Dimani, Hafidh Ally Tahir ukipandishwa kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa Dodoma ili kusafirishwe kwenda Zanzibar kwa mazishi Novemba 11, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

SITTA AIBUA HOJA YA "BUNGE LIVE" MWILI WAKE UKIAGWA DODOMA LEO


Image result for picha za mwili wa sitta
Askari wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu, Samuel Sitta baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam jana. 
 Shughuli za kuaga mwili wa Spika wa Bunge mstaafu Samuel Sitta aliyefariki dunia nchini Ujerumani, leo zitarejesha taratibu wa Bunge kurushwa moja kwa moja (live) kwa kuwa ndiye aliyeasisi utaratibu huo.

Tokea Januari mwaka huu, Bunge la 11 lilizuia kurusha matangazo ya shughuli zake moja kwa moja kwa madai kuwa ni gharama kubwa kufanya hivyo.

Hivi sasa shughuli za Bunge zinazoonyeshwa moja kwa moja ni maswali na majibu na hotuba za mawaziri wakati wa bajeti kuu.

Spika wa Bunge, Job Ndugai jana alitangaza bungeni mara baada ya kuwatambulisha wageni kuwa shughuli hizo zitarushwa moja kwa moja na vyombo vya habari hatua iyolenga katika kumuenzi muasisi wa utaratibu wa kurusha shughuli za Bunge moja kwa moja.

“Kikao hiki maalumu kitakuwa ‘live coverage’ (matangazo ya moja kwa moja) mtindo ambao ulianzishwa chini ya uongozi wake Spika wa kasi na viwango,” alisema Spika Ndugai huku akifunga vifungo vya joho lake la kuongozea Bunge.

Sitta licha ya kuwa mwanzilishi wa Bunge Live, pia alianzisha utaratibu wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu kila siku ya Alhamisi wakati Bunge linapokuwa na mkutano wake, pia utaratibu wa Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali kuongozwa na wabunge kutoka kambi ya upinzani.


Ndugai alisema wabunge wataupokea mwili wa Sitta kwenye Uwanja wa Ndege wa Dodoma, leo saa 8:00 mchana.

Alisema wabunge wote wanatakiwa kuwa wameketi ndani ya Ukumbi wa Bunge tayari kwa kikao hicho maalumu cha Bunge cha kihistoria kitakachoanza saa 8:30 mchana.

Alisema jeneza lenye mwili wa Sitta litawekwa mbele ya kiti cha Spika ndani ya ukumbi huo na kwamba wabunge watatoa salamu za rambirambi.

Spika alisema wabunge wote wataaga mwili huo, ingawa jenezahalitafunguliwa na kuwa shughuli zote za kuaga mwili huo zitafanyika kwa muda wa saa mbili walizopewa.

“Hatua hii itajenga msingi kwa Taifa ambapo viongozi wa kitaifa watakapofariki dunia, miili yao itakuwa ikiagwa kwenye Ukumbi wa Bunge ambako wawakilishi wa Watanzania wote wanapatikana badala ya kwenye Uwanja wa Taifa (jijini Dar es Salaam) na maeneo mengine,” alisema.

Ndugai alisema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe wataongoza katika utoaji wa salamu za rambirambi kwa wabunge.

Alisema baada ya shughuli hiyo jeneza lenye mwili wa Sitta litatolewa nje ya ukumbi huo ili kutoa nafasi ya kutolewa hoja ya kuahirishwa kwa Bunge.

Alisema baada ya kuahirishwa kwa Bunge, wabunge watajipanga nje ya ukumbi huo na kupokezana jeneza hilo hadi kwenye gari litakaloupeleka mwili huo Uwanja wa Ndege wa Dodoma kwa ajili ya kusafirishwa kuelekea Urambo mkoani Tabora kwa ajili ya maziko.

Hata hivyo, alisema wabunge 10 ambao watateuliwa na Tume ya Utumishi ya Bunge kwa uwiano wa vyama watawakilisha Bunge katika shughuli za maziko hayo.

Alisema ujumbe huo utaongozwa na yeye mwenyewe (Ndugai) ambao utaondoka kesho (Jumamosi) na kurejea siku hiyo hiyo mjini Dodoma.

Ili kufanikisha kwa shughuli hiyo aliyoiita ya kihistoria, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu, Jenista Mhagama alitengua vifungu vya kanuni ili kuruhusu mwili na baadhi ya ndugu wa marehemu kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Kanuni za Bunge zilizotenguliwa ili kuruhusu shughuli hiyo ni ni 139 (1), 143 (e) – (f) na 143 ili kuwezesha ndugu na jamaa wa karibu wa marehemu wasiozidi 12 na jeneza lililobeba mwili wa Sitta kuingia ndani ya ukumbi huo.



Samia aongoza waombolezaji

Wakati huohuo; Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan jana aliongoza mamia ya waombolezaji waliofika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kuupokea mwili wa Spika Sitta baada ya kuwasili ukitokea nchini Ujerumani alikofariki dunia kwa ugonjwa wa saratani ya tezi dume.

Mwili wake uliwasili usaa 9:00 jioni kwa Shirika la Ndege la Emirates na kupelekwa nyumbani kwake Masaki Kinondoni ambako utalala.

Simanzi zilitawala uwanjani hapo baada ya Samia kumpokea mjane wa marehemu, Margareth Sitta ambaye alikuwa akimuuguza nchini humo.

Viongozi wengine waliofika kuupokea mwili huo ni Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Seif Ali Idi na Katibu Mkuu Kiongozi, John Kijazi.

Wengine ni Spika wa Bunge mstaafu, Pius Msekwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na baadhi ya mawaziri.

Leo asubuhi mwili wa Sitta utaagwa katika Viwanja vya Karimjee na viongozi mbalimbali wa kitaifa na dini na mchana utaagwa na wabunge mjini Dodoma.

Jumamosi mwili wa Sitta utazikwa wilayani Urambo baada ya kuagwa na ndugu, jamaa na marafiki.

Akizungumza uwanjani hapo, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alikuwapo alisema Taifa limempoteza Sitta ambaye alikuwa mstari wa mbele kupambana na ufisadi. “Nimempoteza kaka yangu na kiongozi ambaye alikuwa mfano wa kuigwa katika nyadhifa alizozishika katika nchi hii,” alisema.

Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka alisema Sitta atakumbukwa kwa kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo.

Alisema mfuko huo ulianzishwa ili kuwawezesha wabunge kuwaletea wananchi maendeleo bila kutegemea fedha za kuomba kutoka kwa matajiri.

Wednesday, November 9, 2016

DSS TV MBEYA A BA LE FANTASTIC 92.7

DSS TV:WANAKULETEA UZINDUZI MKALI WA ALBUM YA VIDEO YA MAN CHENCHELE 13/11/2016 UWANJI HILL MPEMBA



Dss tv inakuletea mfululizo wa mahojiano ya wasanii watakaosindikiza uzinduzi wa Albam ya MAN CHENCHELE kwenye ukumbi wa Uwanji Hill Mpemba juma pili Novemba 13,2016

PRESENTER MR-T HIGHLANDS FM RADIO 
92.7 MHZ 
"SAUTI YAKO"













ANGALIA VIPINDI PIA KWENYE CABLE