Saturday, February 4, 2017

SHEREHE ZA MIAKA 40 YA CCM YAVUNA WANACHAMA 40 KUTOKA CHADEMA TUNDUMA

NA KENNNEDY SIMUMBA DSS TV,  
Sherehe za kuadhimisha miaka 40 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi ambayo yamefanyika mjini Tuduma kwa mikoa miwili ya kiserikali Mbeya na Songwe.
Maadhimisho hayo yamevuma wanachama takribani 40  kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA ambao wamepokelewa na mkuu wa mkoa wa Lindi na mwenyekiti wa CCM Mbeya na Songwe mheshimiwa Godfrey Zambi.Kati ya vijana hao 40 wapo pia makamanda(RB) wa CHADEMA wawili kamanda Ally na kamanda Fidodido kama wanavyoonekana pichani hapo juu.
Akizungumzia ujio wa vijana hao katibu wa siasa na uenezi wa CCM Mbeya na Songwe amesema ni mwanzo wa kulirejesha jimbo la Tunduma 2020. 




No comments:

Post a Comment