Monday, August 29, 2016

MSEMAJI WA CCM AMSIFU LOWASSA

NA KENNEDY SIMUMBA DSS TV,
Msemaji wa chama cha  mapinduzi CCM Christopher Ole Sendeka amesema Lowasa ni muungwana asingekataa kumpa mkono Rais John Magufuli."Namfahamu Lowassa ni muungwana hawezi kuacha kusalimiana kwa kumshika mkono Rais Magufuli.Wamekutana viongozi,Rais na Waziri mkuu mstaafu hawawezi kuacha kusalimiana".Rais Magufuli na Waziri mkuu mstaafu Lowassa walikutana kwenye sherehe ya Jubilee ya miaka 50 ya ndoa ya Rais wa awamu ya tatu mheshimiwa Benjamini William Mkapa iliyofanyika wiki iliyopita.Siku chache zilizopita katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif alikataa kumpa mkono Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi mheshimiwa Dr.Alli Mohamed Shein walipokutana kwenye mazishi ya aliyekuwa Rais wa awamu ya pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Abudi Jumbe.Rais John Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu

No comments:

Post a Comment