Monday, August 29, 2016

YAFAHAMU MATUKIO MAKUBWA MANNE YATAKAYOFANYIKA NCHINI TANZANIA SEPTEMBA MOSI


1.KUPATWA KWA JUA
Tukio la kwanza ni kupatwa kwa jua ambapo tukio hilo litaonekana kwa wakazi wa mikoa ya Mbeya na Njombe.Kwa mjibu wa mamlaka ya utalii nchini wamesema tayari watalii mbalambali 
wameannza kumiminika kwenye mikoa hiyo ili kuweza kushuhudia tukio hilo la kihistoria.
2.JESHI LA ULINZI KUAZIMISHA MIAKA 52 YA MAJESHI SEPTEMBA 1
Tukio la pili ni jeshi la ulinzi la wananchi la Tanzania JWTZ litaazimisha miaka 52 ya majeshi Septemba Mosi.Kwa mjibu wa msemaji wa JWTZ amesema tayari shamrashamra zimeanza
3.MAANDAMANO YA UKUTA
Tukio la tatu ni Chama Cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kufanya maandamano ya Septemba Mosi yaliyopewa jina la UKUTA
Licha ya ktazo kutoka jeshi la polisi nchini lakini bado viongozi wa juu wa chama hicho wameendelea kusisitiza kuwepo kwa maandamano hayo.
 4.WAZIRI MKUU KUHAMIA DODOMA
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa atahamia rasmi Dodoma ambapo anatarajia kuhutubia mkutano mkubwa kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 

No comments:

Post a Comment